Skip to main content

Wanafunzi watengeneza koti linaloweza kuzuia mtu kuvamiwa


Wanafunzi wanne kutoka Mexico wametengeneza koti ambalo wanadai linaweza kuzuia mtu kuvamiwa.

Mikono ya koti hilo linaweza kutoa mshtuko wa umeme utakaomfanya mtu yeyote aliyeligusa kushindwa kutoka.

Wanafunzi hao waliobaini mbinu ya kuwakamata wavamizi wa kijinsia na wamesema walikuja na wazo hilo baada ya kuongezeka kwa idadi kubwa ya watu wanaofanyiwa shambulio la kijinsia katika mji wao.

Aidha wanafunzi hao wamedai kwamba mshtuko huo wa umeme waliouweka kwenye koti ni mdogo hivyo hauwezi kuainishwa kama silaha licha ya kwamba ni imara kuweza kushambulia mtu yeyote.

Koti hilo linaloitwa women wearable lilitengenezwa na Anaid Parra Quiroz na Esthela Gómez ambao ni wanafunzi wa uhandisi na kushirikiana na Giwan Park ambaye ni mwanafunzi wa kutengeza roboti na mwanafunzi wa sheria ambaye ni Guadalupe Martínez.

Wanafunzi hao wanne katika chuo cha Puebla walikuja na wazo hilo ikiwa ni sehemu ya ujasiriamali darasani.

Mamlaka ya mji huo wa Puebla umetoa takwimu zinaonyesha kuwa uvamizi wa kingono unaripotiwa mara tatu kila siku.

Ni namna gani koti hilo linafanya kazi?
Wanafunzi hao walinunua kitambaa cha aina ya kotoni na kuweka ndani betri aina ya 9v katikati ya kitambaa cha ndani na nje,waya hizo zilifungwa vizuri ili lisiweze kumdhuru mvaaji ,vilevile kuna kifungo ambacho unaweza kuwasha na kuzima mtambo huo kwenye koti.

Giwan Park alibuni namna ambavyo mtu anaweza kubonyeza kitufe ambacho lialifanya koti hilo lifanye kazi.

Wakati ambapo koti hilo linaweza kumdhuru mtu ni wakati ambapo mtu anapogusa koti hilo katika mikono wakati mtu anatembea hivyo mshtuo huo wa umeme unaweza kumpata mtu yeyote atayegusa.

Wazo hili liko hivyo ili kumpa nafasi aliyevaa koti muda wa kukimbia au kuwasha kengele

Mwanafunzi wa sheria Guadalupe Martínez aliingia katika utengenezaji wa 'Woman wearable' ili kuhakikisha kuwa hawataenda kinyume na sheria kwa sababu ni chombo cha mtu kujitetea.

Mshtuo huo wa koti ni mdogo hivyo hauwezi kuhatarisha maisha ya mtu yeyote hivyo haijaweza kufikia kiwango cha kuwa silaha.

Koti hilo lilichukua miezi mitatu kulitengeneza .Wanafunzi hao wanasema wangependa kuweka chombo hicho katika maeneo mengine ya koti zaidi ya kwenye mikono.

Hata hivyo chombo hicho kimetengenezwa namna ambavyo inaweza kuwekwa kwenye blause,sketi au suruari.

Wanafunzi wanasema koti hilo linaweza kuuzwa kwa dola 50 au yuro 40.

Comments

Popular posts from this blog

Aina bora za ng’ombe wa maziwa, banda na namna ya kuanza ufugaji

Uzalishaji wa maziwa ni biashara nzuri sana na ya kuvutia ambayo huwa na faida nyingi na humfanya mfugaji kuridhika hasa kwa yule anayependa kazi hii. Hata hivyo, ni lazima kuanza kwa kuweka msingi imara hata kabla ya kufikiria ni aina gani ya mbegu utaichukua kwa ajili ya kufuga. Ni vizuri kufahamu kuwa, usimamizi ni moja ya jambo muhimu sana ambalo likifanyiwa uzembe linaweza hata kumbadilisha ng’ombe wa maziwa kuwa na uzalishaji duni kama ngo’mbe wa kienyeji. Aina mbalimbali za ng’ombe wa maziwa huwa na mahitaji tofauti, hivyo kiwango cha maandalizi yako ni muhimu sana. Unahitajika kufahamu kuwa, unalazimika kufikia mahitaji yako kwa ajili ya lishe, si kwenye mahitaji ya awali tu bali pamoja na mahitaji ya baadaye ya ngo’mbe wako. Suala hili limefanya wafugaji wengi kushindwa kuendelea kutokana na kuwa hujiingiza katika shughuli hii bila kuangalia mambo ya msingi yanayotakiwa pamoja na kuweka mipango thabiti. Pamoja na kuwa mahitaji yote kwa ajili ya lishe na mambo me...

NAJIVUNIA TANZANIA

ZIJUE HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA NA WAKATI MZURI WA KUTEMBELEA   BAADHI YA HIFADHI ZA TAIFA KATIKA PICHA JINSI ZINAVYOONEKANA Na, Gordon Kalulunga WATANZANIA wengi kutokana na mazoea kuwa wanaotakiwa kutembelea hifadhi za Taifa ni watalii wa nje ya nchi, wameshindwa kujitokeza kwa wingi kutembelea hifadhi hizo kutokana na sababu mbalimbali. Moja ya sababu ya kutoweza kutembelea hifadhi hizo ni pamoja na hofu ya viingilio wakifika katika hifadhi hizo jambo ambalo naamini kuwa baada ya kusoma makala hii wengi wetu tutabadili fikra zetu na kujitokeza katika kutembelea vivutia vya utalii vilivyopo kila pembe ya nchi yetu. Baadhi ya vivutio ambavyo vinasimamiwa kikamilifu na Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) ni pamoja na hifadhi ya Taifa ya Arusha, Gombe, Katavi, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Manyara, Ruaha, Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa, Kitulo, Mkomazi na Saanane. Katika Hifadhi hizo za taifa unapotembelea kuna tozo zak...

Mawazo Yakinifu Ya Mafanikio Endelevu Kwako

Mafanikio yoyote yanaanza na mawazo. Hakuna mafanikio yanazaliwa nje ya mawazo. Kwa jinsi unavyokuwa na mawazo bora ndivyo unavyozidi kuwa na mafanikio bora kwako. Mawazo bora unayapata vipi, unayapata kwa kujifunza. Kupitia makala haya, nakukaribisha tujifunze pamoja mawazo yakinifu ya mafanikio yako endelevu. Naamini kupitia mawazo haya, utajifunza kitu ambacho kitakutoa hatua moja na kwenda hatua nyingine, karibu tujifunze. 1.Unaweza ukaendelea kuteseka kila siku na maisha na kuteseka kila na kila aina ya ugonjwa, lakini hiyo yote inaweza ikasababishwa na ujinga ambao  umeushikilia. Ujinga ni adui mkubwa sana wa mafanikio yako. Fanya ufanyalo, futilia mbali ujinga wote ambao upo kwako. Ukifuta ujinga utakuweka huru na utaishi maisha ya mafanikio. Wajinga ndio waliwao na ujinga haumfanikishi mtu, tadhari usiwe kichaka cha ujinga, UTAKWAMA. 2. Kwa mawazo uliyonayo ujue kabisa yanatengeza dunia yako, yanatengeneza maisha yako au yanaumba maisha yako. Swala la kuwa makini sana kw...