Skip to main content

Wanafunzi watengeneza koti linaloweza kuzuia mtu kuvamiwa


Wanafunzi wanne kutoka Mexico wametengeneza koti ambalo wanadai linaweza kuzuia mtu kuvamiwa.

Mikono ya koti hilo linaweza kutoa mshtuko wa umeme utakaomfanya mtu yeyote aliyeligusa kushindwa kutoka.

Wanafunzi hao waliobaini mbinu ya kuwakamata wavamizi wa kijinsia na wamesema walikuja na wazo hilo baada ya kuongezeka kwa idadi kubwa ya watu wanaofanyiwa shambulio la kijinsia katika mji wao.

Aidha wanafunzi hao wamedai kwamba mshtuko huo wa umeme waliouweka kwenye koti ni mdogo hivyo hauwezi kuainishwa kama silaha licha ya kwamba ni imara kuweza kushambulia mtu yeyote.

Koti hilo linaloitwa women wearable lilitengenezwa na Anaid Parra Quiroz na Esthela Gómez ambao ni wanafunzi wa uhandisi na kushirikiana na Giwan Park ambaye ni mwanafunzi wa kutengeza roboti na mwanafunzi wa sheria ambaye ni Guadalupe Martínez.

Wanafunzi hao wanne katika chuo cha Puebla walikuja na wazo hilo ikiwa ni sehemu ya ujasiriamali darasani.

Mamlaka ya mji huo wa Puebla umetoa takwimu zinaonyesha kuwa uvamizi wa kingono unaripotiwa mara tatu kila siku.

Ni namna gani koti hilo linafanya kazi?
Wanafunzi hao walinunua kitambaa cha aina ya kotoni na kuweka ndani betri aina ya 9v katikati ya kitambaa cha ndani na nje,waya hizo zilifungwa vizuri ili lisiweze kumdhuru mvaaji ,vilevile kuna kifungo ambacho unaweza kuwasha na kuzima mtambo huo kwenye koti.

Giwan Park alibuni namna ambavyo mtu anaweza kubonyeza kitufe ambacho lialifanya koti hilo lifanye kazi.

Wakati ambapo koti hilo linaweza kumdhuru mtu ni wakati ambapo mtu anapogusa koti hilo katika mikono wakati mtu anatembea hivyo mshtuo huo wa umeme unaweza kumpata mtu yeyote atayegusa.

Wazo hili liko hivyo ili kumpa nafasi aliyevaa koti muda wa kukimbia au kuwasha kengele

Mwanafunzi wa sheria Guadalupe Martínez aliingia katika utengenezaji wa 'Woman wearable' ili kuhakikisha kuwa hawataenda kinyume na sheria kwa sababu ni chombo cha mtu kujitetea.

Mshtuo huo wa koti ni mdogo hivyo hauwezi kuhatarisha maisha ya mtu yeyote hivyo haijaweza kufikia kiwango cha kuwa silaha.

Koti hilo lilichukua miezi mitatu kulitengeneza .Wanafunzi hao wanasema wangependa kuweka chombo hicho katika maeneo mengine ya koti zaidi ya kwenye mikono.

Hata hivyo chombo hicho kimetengenezwa namna ambavyo inaweza kuwekwa kwenye blause,sketi au suruari.

Wanafunzi wanasema koti hilo linaweza kuuzwa kwa dola 50 au yuro 40.

Comments

Popular posts from this blog

JIFUNZE KALENDA YA UZAZI

Hii ni njia ambayo mwanamke anaweza kutumia kupanga uzazi bila kutumia dawa au kitu cha aina yoyote.  Njia hii inategemea kuchagua kwa makini siku za kufanya mapenzi kutegemeana na ufahamu wa kipindi chote cha hedhi cha mwanamke. Njia hii ina faida yake, lakini yeyote anayeitumia lazima awe makini sana, kwa sababu lazima ajue lini anategemea kupata damu ya hedhi tena.  Ni rahisi sana kufanya makosa kwa kutumia njia hii, kwa hiyo pamoja na kutoa maelezo ya jinsi ya kutumia, sisi hatumshauri mtu kutumia njia hiyo.  Nani anaweza kutumia njia ya kalenda Moja,  Wanawake walioko tayari kuchukua miezi 3 hadi 6 kupima vipindi vyao vya hedhi kabla ya kutumia njia hiyo. Pili,  Wanawake walio na mzunguko wa hedhi ambayo urefu wake haubadiliki. Tatu, Wanawake wanaojua hisabati vizuri sana.  Kwa hiyo, kabla ya kutumia njia hiyo, ni vyema kwa mwanamke kuandaa kalenda inayoonesha siku yake ya kwanza kutoa damu ya hedhi kila mwezi kwa kipindi cha miezi 3 ha...

MAMBO KUMI YA KUFANYA KABLA YA MIAKA 25

1. Jifunze kuweka akiba ya fedha na iache bila kuigusagusa.   2. Tafuta mpenzi sahihi na tulia naye, panga maisha. 3. Ishi mahali pa peke yako, acha kuishi kwa wazazi au kupanga na nyumba na washkaji. 4. Lipa madeni yako ya zamani. Yote! 5. Tengeneza mwili ambao unataka halafu jitahidi kuu-maintain! Anza kuzingatia kuishi kwa kujali afya yako sana. 6. Jitahidi uwe na marafiki ambao wana changamoto za kimaendeleo zitakazokusaidia. 7. Anza kujinunulia assets kama ardhi na nyinginezo. 8. Jifunze kuvaa vizuri na kwa heshima, si tu ilimradi umependeza. 9. Kubali sasa kwamba umekua na acha tabia na mambo ya kitoto. 10. Yaache ya zamani yapite na anza mapya. Mwajuma huna mpango naye, achana naye. Acha kurudi rudi nyuma!

NAJIVUNIA TANZANIA

ZIJUE HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA NA WAKATI MZURI WA KUTEMBELEA   BAADHI YA HIFADHI ZA TAIFA KATIKA PICHA JINSI ZINAVYOONEKANA Na, Gordon Kalulunga WATANZANIA wengi kutokana na mazoea kuwa wanaotakiwa kutembelea hifadhi za Taifa ni watalii wa nje ya nchi, wameshindwa kujitokeza kwa wingi kutembelea hifadhi hizo kutokana na sababu mbalimbali. Moja ya sababu ya kutoweza kutembelea hifadhi hizo ni pamoja na hofu ya viingilio wakifika katika hifadhi hizo jambo ambalo naamini kuwa baada ya kusoma makala hii wengi wetu tutabadili fikra zetu na kujitokeza katika kutembelea vivutia vya utalii vilivyopo kila pembe ya nchi yetu. Baadhi ya vivutio ambavyo vinasimamiwa kikamilifu na Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) ni pamoja na hifadhi ya Taifa ya Arusha, Gombe, Katavi, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Manyara, Ruaha, Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa, Kitulo, Mkomazi na Saanane. Katika Hifadhi hizo za taifa unapotembelea kuna tozo zak...