Skip to main content

Mawazo Yakinifu Ya Mafanikio Endelevu Kwako



Mafanikio yoyote yanaanza na mawazo. Hakuna mafanikio yanazaliwa nje ya mawazo. Kwa jinsi unavyokuwa na mawazo bora ndivyo unavyozidi kuwa na mafanikio bora kwako. Mawazo bora unayapata vipi, unayapata kwa kujifunza.

Kupitia makala haya, nakukaribisha tujifunze pamoja mawazo yakinifu ya mafanikio yako endelevu. Naamini kupitia mawazo haya, utajifunza kitu ambacho kitakutoa hatua moja na kwenda hatua nyingine, karibu tujifunze.

1.Unaweza ukaendelea kuteseka kila siku na maisha na kuteseka kila na kila aina ya ugonjwa, lakini hiyo yote inaweza ikasababishwa na ujinga ambao  umeushikilia. Ujinga ni adui mkubwa sana wa mafanikio yako.

Fanya ufanyalo, futilia mbali ujinga wote ambao upo kwako. Ukifuta ujinga utakuweka huru na utaishi maisha ya mafanikio. Wajinga ndio waliwao na ujinga haumfanikishi mtu, tadhari usiwe kichaka cha ujinga, UTAKWAMA.

2. Kwa mawazo uliyonayo ujue kabisa yanatengeza dunia yako, yanatengeneza maisha yako au yanaumba maisha yako. Swala la kuwa makini sana kwako ni nini ambacho unakiwaza kila wakati.
Kama unawaza upuuzi mwingi, ujue kabisa ndio maisha yako unayabomoa na kuyaharibu kabisa.

Kuwa makini na kile ukiwazacho maana hicho kitaleta matokeo ya maisha yako hata kama matokeo hayo huyapendi.

3. Kama unaona matokeo ya nje yanaathiri maisha yako kwa namna moja au nyingine, basi huhitaji sana kulalamikia matokeo hayo ya nje, bali unachotakiwa kufanya ni kuweka juhudi za kutawala mawazo yako.

Msingi wa maisha yako unaanza na mawazo yako, ukianza kutawaka mawazo yako kwa uhakika na vitu vingine vya nje utavitawala kwa uhakika. Anza kutawala mawazo yako kikamilifu ili ufanikiwe.

4. Kila kitu kinaanzia kwenye mawazo, uzuri au ubaya wa kitu unaanzia kwenye mawazo yako. Kama unaona kitu fulani ni kibaya kwako, kuna mwingine anaonaona kitu hicho ni kizuri kabisa.
Akili yako inaona kutokana na wewe jinsi unavyoamua akili hiyo iweze kuona. Kama unaiona bahari ni sehemu mbaya, wengine wanaona bahari sehemu nzuri ya kuvua samaki, ni suala  la mtazamo wako tu.

5. Furaha ni kitu ambacho unakipata kwanza ndani yako. Furaha kwa lugha nyingine ni uchaguzi ambao wewe unaamua kwamba sasa nataka kuwa na furaha ya namna hii. Furaha si kitu ambacho kinatoka nje yako. Furaha ni wewe unayoiumba ndani yako.

Kama unasubiri hadi ukamilishe mambo fulani hivi, halafu ndio uwe na furaha,  hapo utakuwa ni sawa na kujidanganya. Kwa nini ninasema hivyo ni kwa sababu, furaha ni kitu ambacho ni matokeo ya wewe na si nje yako, fikiri hili na tengeneza furaha yako.

6. Pamoja na kwamba maisha  yanaonekana ni magumu, lakini kipo kitu ambacho unaweza  ukafanya na kitu hicho kikabadili maisha yako na kuwa bora kabisa. Acha kuendelea kukazana kusema maisha ni magumu, fanya kitu.

Kuendelea kukaa tu na kujiimbia wimbo wa maisha ni magumu, hiyo haitakusaidia sana. Amka kutoka kwenye usingizi, amua kuchukua hatua kwa kufanya kitu ambacho kitakutoa kwenye ugumu wa maisha uliopo.

7. Mara nyingi mafanikio makubwa yoyote yale yanakuja kutokana na kufanya mambo ambayo watu wengi hawawezi kufanya. Kama jambo unalolifanya kila mtu analifanya, kufanikiwa kwake inakuwa ni ngumu kwa sababu ya ushindani wake unakuwa mkubwa pia.

Kuwa mtu ambaye unathubutu, kuwa mtu ambaye utajitoa mhanga kufanikisha jambo lile ambalo kila mtu anasema hawezi. Huhitaji maarifa ya ziada au kitu kingine tofauti, ni wewe tu kuamua kujitoa na kusema moyoni mwako kwamba nafanya na naweza pia, DO WHAT CAN’T BE DONE.

8.. Mara nyingi mategemeo bora ya maisha yako ya kesho yanatokana na uzoefu ulionao. Kama kwa siku za hivi karibuni umekuwa na uzoefu mbaya wa kupitia katika hali ngumu ni wazi na lazima utategemea mabaya tu katika maisha yako. Ikiwa lakini umekuwa ukipitia mambo chanya , mategemeo yako yatakuwa pia yapo vizuri.

Dawa pekee itakayoweza kukusaidia wewe uwe na mategemeo mazuri ni kuamua kujilisha dozi kubwa sana ya mambo chanya kwenye maisha kila siku. Kwa kadri unavyozidi kuwa chanya ndivyo mategemeo yako yanazidi kuwa bora. Hakuna mtu ambaye anaweza kuwa na mategemeo bora kama hayuko chanya.

Comments

Popular posts from this blog

JIFUNZE KALENDA YA UZAZI

Hii ni njia ambayo mwanamke anaweza kutumia kupanga uzazi bila kutumia dawa au kitu cha aina yoyote.  Njia hii inategemea kuchagua kwa makini siku za kufanya mapenzi kutegemeana na ufahamu wa kipindi chote cha hedhi cha mwanamke. Njia hii ina faida yake, lakini yeyote anayeitumia lazima awe makini sana, kwa sababu lazima ajue lini anategemea kupata damu ya hedhi tena.  Ni rahisi sana kufanya makosa kwa kutumia njia hii, kwa hiyo pamoja na kutoa maelezo ya jinsi ya kutumia, sisi hatumshauri mtu kutumia njia hiyo.  Nani anaweza kutumia njia ya kalenda Moja,  Wanawake walioko tayari kuchukua miezi 3 hadi 6 kupima vipindi vyao vya hedhi kabla ya kutumia njia hiyo. Pili,  Wanawake walio na mzunguko wa hedhi ambayo urefu wake haubadiliki. Tatu, Wanawake wanaojua hisabati vizuri sana.  Kwa hiyo, kabla ya kutumia njia hiyo, ni vyema kwa mwanamke kuandaa kalenda inayoonesha siku yake ya kwanza kutoa damu ya hedhi kila mwezi kwa kipindi cha miezi 3 ha...

MAMBO KUMI YA KUFANYA KABLA YA MIAKA 25

1. Jifunze kuweka akiba ya fedha na iache bila kuigusagusa.   2. Tafuta mpenzi sahihi na tulia naye, panga maisha. 3. Ishi mahali pa peke yako, acha kuishi kwa wazazi au kupanga na nyumba na washkaji. 4. Lipa madeni yako ya zamani. Yote! 5. Tengeneza mwili ambao unataka halafu jitahidi kuu-maintain! Anza kuzingatia kuishi kwa kujali afya yako sana. 6. Jitahidi uwe na marafiki ambao wana changamoto za kimaendeleo zitakazokusaidia. 7. Anza kujinunulia assets kama ardhi na nyinginezo. 8. Jifunze kuvaa vizuri na kwa heshima, si tu ilimradi umependeza. 9. Kubali sasa kwamba umekua na acha tabia na mambo ya kitoto. 10. Yaache ya zamani yapite na anza mapya. Mwajuma huna mpango naye, achana naye. Acha kurudi rudi nyuma!

NAJIVUNIA TANZANIA

ZIJUE HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA NA WAKATI MZURI WA KUTEMBELEA   BAADHI YA HIFADHI ZA TAIFA KATIKA PICHA JINSI ZINAVYOONEKANA Na, Gordon Kalulunga WATANZANIA wengi kutokana na mazoea kuwa wanaotakiwa kutembelea hifadhi za Taifa ni watalii wa nje ya nchi, wameshindwa kujitokeza kwa wingi kutembelea hifadhi hizo kutokana na sababu mbalimbali. Moja ya sababu ya kutoweza kutembelea hifadhi hizo ni pamoja na hofu ya viingilio wakifika katika hifadhi hizo jambo ambalo naamini kuwa baada ya kusoma makala hii wengi wetu tutabadili fikra zetu na kujitokeza katika kutembelea vivutia vya utalii vilivyopo kila pembe ya nchi yetu. Baadhi ya vivutio ambavyo vinasimamiwa kikamilifu na Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) ni pamoja na hifadhi ya Taifa ya Arusha, Gombe, Katavi, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Manyara, Ruaha, Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa, Kitulo, Mkomazi na Saanane. Katika Hifadhi hizo za taifa unapotembelea kuna tozo zak...