Skip to main content

Kanuni 29 za kuishi na Watu / Binadam Vizuri

Mojawapo ya mambo muhimu katika mafanikio ya aina yoyote maishani ni kupata msaada wa aina Fulani kutoka kwa watu wengine. Mtu hawezi kufanikiwa bila msaada wa watu,kwa maana hakuna mtu anayejua kila kitu/jambo na anayeweza kufanya kila kitu Duniani.

 Kwa namna yeyote ile mtu anahitaji msaada wa wengine. Hivyo ili kupata msaada wa wengine ni lazima kujua namna ya kuishi na watu vizuri.Ingawa siyo rahisi kumpendeza kila mtu, lakini watu wengi utaishi nao kwa amani.

Zifuatazo ni KANUNI na MBINU mhimu za kuishi na watu vizuri.
1: Uwe na tabia ya kupenda watu kwa moyo wote,hali kadhalika na wewe watakupenda.
2: Heshimu kila mtu na kila mtu umwone ni muhimu sana na wa maana.
3: Usimdharau mtu yeyote kutokana na hali yake,hata akiwa ni masikini ,hakuelimika,hana cheo cha       juu na kadhalika.
4: Uwe mtu wa furaha na tabasamu unapokutana na watu.
5: Uwe mcheshi na mtu ambaye watu wanafurahi kuwa nawe.
6: Usipende kulaumu watu na kama utalaumu mtu,tumia njia nzuri na ya upole ya kumsaidia na              kumjenga.
7: Usiwe msengenyaji na usimseme mtu vibaya.
8: Usipende kugombeza na kutukana au kutoa matusi kwa watu.
9: Shukru kwa kila jambo jema linapotendeka kwa kusema ahsante au shukru kwa kila jambo._
10: Usiwe mtu wa kujipendekeza kwa watu au wakubwa.
11: Usipende mabishano na kama yakitokea,usitake kila mara kushinda.
12: Uwe mpole na usiwe mkali kwa watu.
13: Usipende kugombana,kupiga au kupigana na watu.
14: Uwe mnyenyekevu na usijivune kwa kwa lolote lile,kama kuna jambo zuri kwako acha wengine         wakusifu.
15: Usiwe na kinyongo,fitina na usitunze chuki.
16: Usilipize kisasi,badala yake tenda wema kwa Yule anayekukosea.
17: Usiwe unachonganisha watu,ukiambiwa udhaifu wa mtu usiende kumwambia aliyesema.
18: Jipende na kujikubali kama ulivyo kimaumbile na uwezo wako,ndipo na watu nao watakupenda         na kukubali kama ulivyo.
19: Tunza siri zako na za wengine.
20: Usiwe mwepesi wa hasira
21: Kumbuka majina ya watu unaokutana nao.
22: Usiwe mzungumzaji kupita kiasi,badala yake uwe msikilizaji mzuri.
23: Usiseme uongo au kuongeza chumvi au kupotosha ukweli.
24: Zungumza kufuatana na mambo mtu anayoyapenda.
25: Maliza ugomvi au migogoro na wengine kwa njia ya amani kwa kuzungumza na mhusika.
26: Jifunze kusamehe makosa ya watu.
27: Unapofanya makosa,kubali na kuungama na kuomba msamaha.
28: Heshimu na kuvumilia mawazo na maoni ya wengine ambayo ni tofauti na yako.
29: Nigongee like hata kama hujaipenda hii.

Comments

Popular posts from this blog

Aina bora za ng’ombe wa maziwa, banda na namna ya kuanza ufugaji

Uzalishaji wa maziwa ni biashara nzuri sana na ya kuvutia ambayo huwa na faida nyingi na humfanya mfugaji kuridhika hasa kwa yule anayependa kazi hii. Hata hivyo, ni lazima kuanza kwa kuweka msingi imara hata kabla ya kufikiria ni aina gani ya mbegu utaichukua kwa ajili ya kufuga. Ni vizuri kufahamu kuwa, usimamizi ni moja ya jambo muhimu sana ambalo likifanyiwa uzembe linaweza hata kumbadilisha ng’ombe wa maziwa kuwa na uzalishaji duni kama ngo’mbe wa kienyeji. Aina mbalimbali za ng’ombe wa maziwa huwa na mahitaji tofauti, hivyo kiwango cha maandalizi yako ni muhimu sana. Unahitajika kufahamu kuwa, unalazimika kufikia mahitaji yako kwa ajili ya lishe, si kwenye mahitaji ya awali tu bali pamoja na mahitaji ya baadaye ya ngo’mbe wako. Suala hili limefanya wafugaji wengi kushindwa kuendelea kutokana na kuwa hujiingiza katika shughuli hii bila kuangalia mambo ya msingi yanayotakiwa pamoja na kuweka mipango thabiti. Pamoja na kuwa mahitaji yote kwa ajili ya lishe na mambo me...

NAJIVUNIA TANZANIA

ZIJUE HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA NA WAKATI MZURI WA KUTEMBELEA   BAADHI YA HIFADHI ZA TAIFA KATIKA PICHA JINSI ZINAVYOONEKANA Na, Gordon Kalulunga WATANZANIA wengi kutokana na mazoea kuwa wanaotakiwa kutembelea hifadhi za Taifa ni watalii wa nje ya nchi, wameshindwa kujitokeza kwa wingi kutembelea hifadhi hizo kutokana na sababu mbalimbali. Moja ya sababu ya kutoweza kutembelea hifadhi hizo ni pamoja na hofu ya viingilio wakifika katika hifadhi hizo jambo ambalo naamini kuwa baada ya kusoma makala hii wengi wetu tutabadili fikra zetu na kujitokeza katika kutembelea vivutia vya utalii vilivyopo kila pembe ya nchi yetu. Baadhi ya vivutio ambavyo vinasimamiwa kikamilifu na Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) ni pamoja na hifadhi ya Taifa ya Arusha, Gombe, Katavi, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Manyara, Ruaha, Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa, Kitulo, Mkomazi na Saanane. Katika Hifadhi hizo za taifa unapotembelea kuna tozo zak...

How to write a CV: Tips for 2018 (with examples)

When it comes to job hunting, your CV is paramount. Get it right, and you’ll have an interview in no time, but get it wrong, and you may face rejection after rejection. Every CV is different as you want to show why your set of skills makes you suitable for the position you’re applying for at that moment, but all follow a similar structure. This guide will show you how to write a great CV that’s ready for 2018 and beyond. What is a CV? Your CV, short for curriculum vitae ,  is a personal marketing document used to sell yourself to prospective employers. It should tell them about you, your professional history and your skills, abilities and achievements. Ultimately, it should highlight why you’re the best person for the job. A CV is required when applying for a job. In addition to your CV, employers may also require a cover letter and a completed application form( Browse CV templates ) What to include in your CV in 2018 While the structure of a CV is flexible, bending t...