Skip to main content



MABINGWA wa Kombe la SportPesa, Gor Mahia kutoka Kenya wanatarajia kuikaribisha Everton FC inayoshiriki Ligi Kuu England katika mechi ya kirafiki itakayopigwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam-

huku mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Wayne Rooney akisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka wa Tanzania.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Harrison Mwakyembe, jana aliongoza viongozi mbalimbali wa serikali na wadau wa soka nchini waliojitokeza kuipokea timu hiyo ambayo imekuja nchini kwa mwaliko wa Kampuni ya SportPesa Tanzania.

Mechi ya leo itakuwa ni ya kwanza kwa Rooney tangu arejee katika klabu yake hiyo akitokea Manchester United ambayo aliitumikia kwa miaka 13.

Kocha wa Everton, Ronald Koeman, alisema kuwa kila mchezaji wa timu hiyo ambaye amekuja nchini atapata muda wa kucheza kuanzia dakika 45 na wataondoka kesho.

"Hii ndiyo mechi ya kwanza ya kirafiki na kila mchezaji nitampatia dakika 45. Tunacheza mpira kwa ajili ya kushindana, tunatarajia kupata ushindi katika mchezo huu utakaofanyika Tanzania," alisema.

Kocha Mkuu wa Gor Mahia, Dylan Kerr, alisema jana kuwa timu yake imejipanga kuitumia vizuri nafasi ya kucheza na Everton ambayo ina wachezaji wanaoshiriki moja ya ligi zenye kiwango cha juu duniani.

“Ninatumaini tutatumia vizuri nafasi hii kama ambavyo tulionyesha uwezo wetu na kuibuka washindi katika mashindano ya Kombe la SportPesa, hakuna timu ndogo katika dunia ya sasa, mpira ni uwanjani na si jina au taifa la mchezaji linalohusika kwenye mchezo,” alisema Kerr, kocha wa zamani wa Simba.

Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Alfred Lucas, alisema jana kuwa maandalizi ya mchezo huo yamekamilika na waamuzi wa hapa nchini wakiongozwa na Israel Nkongo, Fredinand Chacha na Frank Komba ambao wana beji zinazotambulika na Fifa ndiyo watachezesha mechi hiyo.

Alimtaja Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, ndiye atakuwa mgeni rasmi katika mechi hiyo inayotarajiwa kuanza saa 11:00 jioni
huku kiingilio cha chini kikiwa ni Sh. 3,000.kemege.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

NAJIVUNIA TANZANIA

ZIJUE HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA NA WAKATI MZURI WA KUTEMBELEA   BAADHI YA HIFADHI ZA TAIFA KATIKA PICHA JINSI ZINAVYOONEKANA Na, Gordon Kalulunga WATANZANIA wengi kutokana na mazoea kuwa wanaotakiwa kutembelea hifadhi za Taifa ni watalii wa nje ya nchi, wameshindwa kujitokeza kwa wingi kutembelea hifadhi hizo kutokana na sababu mbalimbali. Moja ya sababu ya kutoweza kutembelea hifadhi hizo ni pamoja na hofu ya viingilio wakifika katika hifadhi hizo jambo ambalo naamini kuwa baada ya kusoma makala hii wengi wetu tutabadili fikra zetu na kujitokeza katika kutembelea vivutia vya utalii vilivyopo kila pembe ya nchi yetu. Baadhi ya vivutio ambavyo vinasimamiwa kikamilifu na Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) ni pamoja na hifadhi ya Taifa ya Arusha, Gombe, Katavi, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Manyara, Ruaha, Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa, Kitulo, Mkomazi na Saanane. Katika Hifadhi hizo za taifa unapotembelea kuna tozo zak...

MAMBO KUMI YA KUFANYA KABLA YA MIAKA 25

1. Jifunze kuweka akiba ya fedha na iache bila kuigusagusa.   2. Tafuta mpenzi sahihi na tulia naye, panga maisha. 3. Ishi mahali pa peke yako, acha kuishi kwa wazazi au kupanga na nyumba na washkaji. 4. Lipa madeni yako ya zamani. Yote! 5. Tengeneza mwili ambao unataka halafu jitahidi kuu-maintain! Anza kuzingatia kuishi kwa kujali afya yako sana. 6. Jitahidi uwe na marafiki ambao wana changamoto za kimaendeleo zitakazokusaidia. 7. Anza kujinunulia assets kama ardhi na nyinginezo. 8. Jifunze kuvaa vizuri na kwa heshima, si tu ilimradi umependeza. 9. Kubali sasa kwamba umekua na acha tabia na mambo ya kitoto. 10. Yaache ya zamani yapite na anza mapya. Mwajuma huna mpango naye, achana naye. Acha kurudi rudi nyuma!

How to write a CV: Tips for 2018 (with examples)

When it comes to job hunting, your CV is paramount. Get it right, and you’ll have an interview in no time, but get it wrong, and you may face rejection after rejection. Every CV is different as you want to show why your set of skills makes you suitable for the position you’re applying for at that moment, but all follow a similar structure. This guide will show you how to write a great CV that’s ready for 2018 and beyond. What is a CV? Your CV, short for curriculum vitae ,  is a personal marketing document used to sell yourself to prospective employers. It should tell them about you, your professional history and your skills, abilities and achievements. Ultimately, it should highlight why you’re the best person for the job. A CV is required when applying for a job. In addition to your CV, employers may also require a cover letter and a completed application form( Browse CV templates ) What to include in your CV in 2018 While the structure of a CV is flexible, bending t...