Skip to main content

NJIA ZA MAFANIKIO

Miongoni mwa kauli ambazo nilikuwa nasikia wakati nakua nilikuwa nasikia wanasema maisha ni kama kioo ukicheka na yenyewe yanacheka. Kwa kipindi hicho sikuwahi kujua wanamaana gani watu waliyokuwa wanasema hivyo. Ila kwa bahati nzuri siku zinavyozidi kwenda ndivyo ninavyoelewa walikuwa wanamaanisha nini.

Kwa utafiti wangu nimegundua ya kwamba katika maisha ya kusaka mafanikio ni lazima ujishughulishe kwa kutumia nguvu, kipaji, juhudi na maarifa ili uweze kupata mafanikio hayo. Na endapo utafanya kinyume chache utazidi kulaumu na kuishia kusema ndoto zangu ni kuwa mtu fulani na vitu kama hivyo.

Mwandishi mmoja anayeitwa Charles Nduku aliwahi kuandika katika kitabu chake cha ‘my plan, my life’ kwa kusema acha Kuota ndoto bali anza kufanya.

Kwa kipindi kirefu umekuwa unasema nataka kuwa hivi na vile. Kumbuka ya kwamba huu sio mda wa kusema maneno hayo. Ila muda wakuanza kutekeleza malengo yako. Watu wengi wapo vizuri zaidi kwa kusema kuliko kutenda, na ukichunguza vizuri watu hao hufa na ndoto zao. Badili mtazamo wako na kuwa ni mtu wa vitendo dhidi ya maneno.

Utaweza kubadili mtazamo wako na kuwa mtu wa vitendo ikiwa lakini utajifunza kutumia njia huru za kimafanikio. Kwa kusoma makala haya utajifunza njia hizo huru za mafanikio ambazo zitakufanya ufanikiwe. Naamini una hamu ya kutaka kuelewa ni njia zipi huru za mafanikio ambazo unaweza kuzitumia. Karibu na twende pamoja kujifunza njia hizo.

1. Tafuta nafasi.
Kwa kile ambacho unataka kuwa tafuta nafasi ya kutenda jambo hilo. Watu wengi kama niliposema hapo awali ni wazuri wa kusema kuliko kutenda. Kwa mfano kuna watu wanasema nataka kuwa muigizaji utamsikia akisema tu nataka kuwa muigizaji ila hatafuti nafasi ya kuwa muigizaji. Halikadharika hata wewe mwenye kitu cha tofauti, fanya kitu hicho na usiishie kusema tu haitakusaidia. Endapo utaishia kusema tu jiandae kufa na malengo yako.

Katika kutafuta nafasi ni lazima ujiulize nafasi hiyo ninayo au sina , kama sina naipata wapi? Ni nini kitu ambacho kinahitajika katika nafasi hiyo ninacho au sina kama sina nina kipata wapi? Ukipata majibu ya maswali hayo lazima uweze kufanikiwa.

2. Tengeneza jina.
Katika jambo ambalo unalifanya ni lazima utengeneze jina ambalo watu wataweza kukufahamu kwa kile ambacho unakifanya.

Utengezaji wa jina hutokana na kutengeneza huduma bora kwa watu wengine. Kwa mfano kuna siku nilikuwa katika harakati zangu za hapa na pale nikawa akapita mtoto mdogo ni kamuuliza yule mtoto et nitapata wapi chipsi mtoto yule akanijibu nenda kwa mpemba, wakati najiuliza ni kitu gani kinamfanya huyo mpemba mpaka watoto wadogo wamfahamu, nilipofika hapo kwa huyo mpemba ndipo nilipopata jibu. Ya kuwa ubora na usafi wake ndio uliomfanya atengeneze jina. Jina hilo ndilo linalomtengenezea wataja wengi.

Nadhani pia utakuwa unawafahamu watu wenye majina makubwa ambao wanazalisha vitu vyenye ubora kwa hapa nchini. Kama ndivyo hivyo ni wakati wako na wewe kuweza kutengeneza jina kwa jambo ambalo unalifanya. Ifike wakati mtu akitaka kitu fulani hata ukimuuliza mtu yeyote hata awe mtoto mdogo awe anakufahamu kutoka na kile unachokifanya.

Kama ilivyo leo kwa watu wengi maarufu unaowafahamu..
Ukiyafanya hayo hapo ndipo pesa zitapokuja kwa kasi zaidi. Mbinu hizo huru za kimafanikio wengi waliofanikwa ndizo ambazo walizozitumia. Zitumie leo uwe tajiri mkubwa.

Comments

Popular posts from this blog

Aina bora za ng’ombe wa maziwa, banda na namna ya kuanza ufugaji

Uzalishaji wa maziwa ni biashara nzuri sana na ya kuvutia ambayo huwa na faida nyingi na humfanya mfugaji kuridhika hasa kwa yule anayependa kazi hii. Hata hivyo, ni lazima kuanza kwa kuweka msingi imara hata kabla ya kufikiria ni aina gani ya mbegu utaichukua kwa ajili ya kufuga. Ni vizuri kufahamu kuwa, usimamizi ni moja ya jambo muhimu sana ambalo likifanyiwa uzembe linaweza hata kumbadilisha ng’ombe wa maziwa kuwa na uzalishaji duni kama ngo’mbe wa kienyeji. Aina mbalimbali za ng’ombe wa maziwa huwa na mahitaji tofauti, hivyo kiwango cha maandalizi yako ni muhimu sana. Unahitajika kufahamu kuwa, unalazimika kufikia mahitaji yako kwa ajili ya lishe, si kwenye mahitaji ya awali tu bali pamoja na mahitaji ya baadaye ya ngo’mbe wako. Suala hili limefanya wafugaji wengi kushindwa kuendelea kutokana na kuwa hujiingiza katika shughuli hii bila kuangalia mambo ya msingi yanayotakiwa pamoja na kuweka mipango thabiti. Pamoja na kuwa mahitaji yote kwa ajili ya lishe na mambo me...

NAJIVUNIA TANZANIA

ZIJUE HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA NA WAKATI MZURI WA KUTEMBELEA   BAADHI YA HIFADHI ZA TAIFA KATIKA PICHA JINSI ZINAVYOONEKANA Na, Gordon Kalulunga WATANZANIA wengi kutokana na mazoea kuwa wanaotakiwa kutembelea hifadhi za Taifa ni watalii wa nje ya nchi, wameshindwa kujitokeza kwa wingi kutembelea hifadhi hizo kutokana na sababu mbalimbali. Moja ya sababu ya kutoweza kutembelea hifadhi hizo ni pamoja na hofu ya viingilio wakifika katika hifadhi hizo jambo ambalo naamini kuwa baada ya kusoma makala hii wengi wetu tutabadili fikra zetu na kujitokeza katika kutembelea vivutia vya utalii vilivyopo kila pembe ya nchi yetu. Baadhi ya vivutio ambavyo vinasimamiwa kikamilifu na Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) ni pamoja na hifadhi ya Taifa ya Arusha, Gombe, Katavi, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Manyara, Ruaha, Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa, Kitulo, Mkomazi na Saanane. Katika Hifadhi hizo za taifa unapotembelea kuna tozo zak...

How to write a CV: Tips for 2018 (with examples)

When it comes to job hunting, your CV is paramount. Get it right, and you’ll have an interview in no time, but get it wrong, and you may face rejection after rejection. Every CV is different as you want to show why your set of skills makes you suitable for the position you’re applying for at that moment, but all follow a similar structure. This guide will show you how to write a great CV that’s ready for 2018 and beyond. What is a CV? Your CV, short for curriculum vitae ,  is a personal marketing document used to sell yourself to prospective employers. It should tell them about you, your professional history and your skills, abilities and achievements. Ultimately, it should highlight why you’re the best person for the job. A CV is required when applying for a job. In addition to your CV, employers may also require a cover letter and a completed application form( Browse CV templates ) What to include in your CV in 2018 While the structure of a CV is flexible, bending t...