Skip to main content

Wabunge wawapongeza watoto wa Kikwete, Nkamia



Wanafunzi watatu walioshinda tuzo ya Genius Olympiad huko Marekani wametambulishwa bungeni jana kwa kuliletea Taifa heshima.

Wanafunzi hao kutoka Sekondari ya Wavulana ya Feza jijini Dar es Salaam waliambatana na walimu wao wawili. Walikuja bungeni kwa mwaliko wa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako.

Spika wa Bunge, Job Ndugai aliwatambulisha wageni watano wa Profesa Ndalichako wakiwamo walimu wawili na wanafunzi watatu walioshinda medali za dhahabu katika mashindano ya kimataifa ya mazingira na sayansi yaliyofanyika.

“Tunawapongeza kwa kushinda tuzo hizo. Mmepeperusha bendera ya Tanzania vizuri sana,” alisema Ndugai.

Aliwataja wanafunzi hao kuwa ni Abdallah Rubeya, Abdularazak Juma Nkamia ambaye ni mtoto wa Mbunge wa Chemba, Juma Nkamia na Khalifan Jakaya Kikwete, mtoto wa Rais mstaafu, Jakaya Kikwete.

Hakusita kutania na kuwapongeza wazazi wa watoto hao kwa kusema: “Kutoka Chemba mpaka Marekani na kufanya mambo kule, kumbe inawezekana haya mambo. Lakini, hongera sana kwa Mama Salma Kikwete kwa sababu yupo Khalfan Jakaya Kikwete.”

Kukaribishwa kwao bungeni ni sehemu ya juhudi za Serikali kuwatambua wanafunzi wanaofanya vizuri kwenye masomo yao ili kuwaongezea morali na kuwahamasisha wengine waliopo kwenye ngazi tofauti shuleni na vyuoni pia.

Hivi karibuni, watoto hao walipokelewa kishujaa na ndugu, jamaa na marafiki waliojitokeza Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam kabla hawajaletwa bungeni jana.

Walioongozana na wanafunzi hao ni mkurugenzi pamoja na mkuu wa shule hiyo

Comments

Popular posts from this blog

NAJIVUNIA TANZANIA

ZIJUE HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA NA WAKATI MZURI WA KUTEMBELEA   BAADHI YA HIFADHI ZA TAIFA KATIKA PICHA JINSI ZINAVYOONEKANA Na, Gordon Kalulunga WATANZANIA wengi kutokana na mazoea kuwa wanaotakiwa kutembelea hifadhi za Taifa ni watalii wa nje ya nchi, wameshindwa kujitokeza kwa wingi kutembelea hifadhi hizo kutokana na sababu mbalimbali. Moja ya sababu ya kutoweza kutembelea hifadhi hizo ni pamoja na hofu ya viingilio wakifika katika hifadhi hizo jambo ambalo naamini kuwa baada ya kusoma makala hii wengi wetu tutabadili fikra zetu na kujitokeza katika kutembelea vivutia vya utalii vilivyopo kila pembe ya nchi yetu. Baadhi ya vivutio ambavyo vinasimamiwa kikamilifu na Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) ni pamoja na hifadhi ya Taifa ya Arusha, Gombe, Katavi, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Manyara, Ruaha, Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa, Kitulo, Mkomazi na Saanane. Katika Hifadhi hizo za taifa unapotembelea kuna tozo zak...

MAMBO KUMI YA KUFANYA KABLA YA MIAKA 25

1. Jifunze kuweka akiba ya fedha na iache bila kuigusagusa.   2. Tafuta mpenzi sahihi na tulia naye, panga maisha. 3. Ishi mahali pa peke yako, acha kuishi kwa wazazi au kupanga na nyumba na washkaji. 4. Lipa madeni yako ya zamani. Yote! 5. Tengeneza mwili ambao unataka halafu jitahidi kuu-maintain! Anza kuzingatia kuishi kwa kujali afya yako sana. 6. Jitahidi uwe na marafiki ambao wana changamoto za kimaendeleo zitakazokusaidia. 7. Anza kujinunulia assets kama ardhi na nyinginezo. 8. Jifunze kuvaa vizuri na kwa heshima, si tu ilimradi umependeza. 9. Kubali sasa kwamba umekua na acha tabia na mambo ya kitoto. 10. Yaache ya zamani yapite na anza mapya. Mwajuma huna mpango naye, achana naye. Acha kurudi rudi nyuma!

How to write a CV: Tips for 2018 (with examples)

When it comes to job hunting, your CV is paramount. Get it right, and you’ll have an interview in no time, but get it wrong, and you may face rejection after rejection. Every CV is different as you want to show why your set of skills makes you suitable for the position you’re applying for at that moment, but all follow a similar structure. This guide will show you how to write a great CV that’s ready for 2018 and beyond. What is a CV? Your CV, short for curriculum vitae ,  is a personal marketing document used to sell yourself to prospective employers. It should tell them about you, your professional history and your skills, abilities and achievements. Ultimately, it should highlight why you’re the best person for the job. A CV is required when applying for a job. In addition to your CV, employers may also require a cover letter and a completed application form( Browse CV templates ) What to include in your CV in 2018 While the structure of a CV is flexible, bending t...