Skip to main content

Wabunge wawapongeza watoto wa Kikwete, Nkamia



Wanafunzi watatu walioshinda tuzo ya Genius Olympiad huko Marekani wametambulishwa bungeni jana kwa kuliletea Taifa heshima.

Wanafunzi hao kutoka Sekondari ya Wavulana ya Feza jijini Dar es Salaam waliambatana na walimu wao wawili. Walikuja bungeni kwa mwaliko wa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako.

Spika wa Bunge, Job Ndugai aliwatambulisha wageni watano wa Profesa Ndalichako wakiwamo walimu wawili na wanafunzi watatu walioshinda medali za dhahabu katika mashindano ya kimataifa ya mazingira na sayansi yaliyofanyika.

“Tunawapongeza kwa kushinda tuzo hizo. Mmepeperusha bendera ya Tanzania vizuri sana,” alisema Ndugai.

Aliwataja wanafunzi hao kuwa ni Abdallah Rubeya, Abdularazak Juma Nkamia ambaye ni mtoto wa Mbunge wa Chemba, Juma Nkamia na Khalifan Jakaya Kikwete, mtoto wa Rais mstaafu, Jakaya Kikwete.

Hakusita kutania na kuwapongeza wazazi wa watoto hao kwa kusema: “Kutoka Chemba mpaka Marekani na kufanya mambo kule, kumbe inawezekana haya mambo. Lakini, hongera sana kwa Mama Salma Kikwete kwa sababu yupo Khalfan Jakaya Kikwete.”

Kukaribishwa kwao bungeni ni sehemu ya juhudi za Serikali kuwatambua wanafunzi wanaofanya vizuri kwenye masomo yao ili kuwaongezea morali na kuwahamasisha wengine waliopo kwenye ngazi tofauti shuleni na vyuoni pia.

Hivi karibuni, watoto hao walipokelewa kishujaa na ndugu, jamaa na marafiki waliojitokeza Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam kabla hawajaletwa bungeni jana.

Walioongozana na wanafunzi hao ni mkurugenzi pamoja na mkuu wa shule hiyo

Comments

Popular posts from this blog

Aina bora za ng’ombe wa maziwa, banda na namna ya kuanza ufugaji

Uzalishaji wa maziwa ni biashara nzuri sana na ya kuvutia ambayo huwa na faida nyingi na humfanya mfugaji kuridhika hasa kwa yule anayependa kazi hii. Hata hivyo, ni lazima kuanza kwa kuweka msingi imara hata kabla ya kufikiria ni aina gani ya mbegu utaichukua kwa ajili ya kufuga. Ni vizuri kufahamu kuwa, usimamizi ni moja ya jambo muhimu sana ambalo likifanyiwa uzembe linaweza hata kumbadilisha ng’ombe wa maziwa kuwa na uzalishaji duni kama ngo’mbe wa kienyeji. Aina mbalimbali za ng’ombe wa maziwa huwa na mahitaji tofauti, hivyo kiwango cha maandalizi yako ni muhimu sana. Unahitajika kufahamu kuwa, unalazimika kufikia mahitaji yako kwa ajili ya lishe, si kwenye mahitaji ya awali tu bali pamoja na mahitaji ya baadaye ya ngo’mbe wako. Suala hili limefanya wafugaji wengi kushindwa kuendelea kutokana na kuwa hujiingiza katika shughuli hii bila kuangalia mambo ya msingi yanayotakiwa pamoja na kuweka mipango thabiti. Pamoja na kuwa mahitaji yote kwa ajili ya lishe na mambo me...

NAJIVUNIA TANZANIA

ZIJUE HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA NA WAKATI MZURI WA KUTEMBELEA   BAADHI YA HIFADHI ZA TAIFA KATIKA PICHA JINSI ZINAVYOONEKANA Na, Gordon Kalulunga WATANZANIA wengi kutokana na mazoea kuwa wanaotakiwa kutembelea hifadhi za Taifa ni watalii wa nje ya nchi, wameshindwa kujitokeza kwa wingi kutembelea hifadhi hizo kutokana na sababu mbalimbali. Moja ya sababu ya kutoweza kutembelea hifadhi hizo ni pamoja na hofu ya viingilio wakifika katika hifadhi hizo jambo ambalo naamini kuwa baada ya kusoma makala hii wengi wetu tutabadili fikra zetu na kujitokeza katika kutembelea vivutia vya utalii vilivyopo kila pembe ya nchi yetu. Baadhi ya vivutio ambavyo vinasimamiwa kikamilifu na Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) ni pamoja na hifadhi ya Taifa ya Arusha, Gombe, Katavi, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Manyara, Ruaha, Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa, Kitulo, Mkomazi na Saanane. Katika Hifadhi hizo za taifa unapotembelea kuna tozo zak...

How to write a CV: Tips for 2018 (with examples)

When it comes to job hunting, your CV is paramount. Get it right, and you’ll have an interview in no time, but get it wrong, and you may face rejection after rejection. Every CV is different as you want to show why your set of skills makes you suitable for the position you’re applying for at that moment, but all follow a similar structure. This guide will show you how to write a great CV that’s ready for 2018 and beyond. What is a CV? Your CV, short for curriculum vitae ,  is a personal marketing document used to sell yourself to prospective employers. It should tell them about you, your professional history and your skills, abilities and achievements. Ultimately, it should highlight why you’re the best person for the job. A CV is required when applying for a job. In addition to your CV, employers may also require a cover letter and a completed application form( Browse CV templates ) What to include in your CV in 2018 While the structure of a CV is flexible, bending t...