Skip to main content

Ulinzi wa madini BoT wahojiwa

WABUNGE wameibana serikali ieleze maandalizi yake kwenye ulinzi wa hifadhi ya madini itakayokuwa kwenye Benki Kuu (BoT) kabla ya kuyauza.

Hatua hiyo ilitokana na Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi kuwasilisha maelezo ya serikali kuhusu Muswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa mwaka 2017, kwa Kamati ya Katiba na Sheria juzi mjini hapa.

Miongoni mwa wabunge waliohoji ni pamoja na Mbunge wa Newala Vijijini (CCM), Rashid Akibar akibainisha kuwa hapo awali BoT iliwahi kutunza dhahabu na baada ya muda vikautwaa mchanga na si dhahabu tena. Alitaka waziri Kabudi atoa ufafanuzi wa jambo hilo.

“Serikali iko tayari kuchukua ulinzi nchini Marekani?” Alihoji mbunge huyo.

Naye Mbunge wa Tarime Mjini (Chadema), John Heche alisema jengo la BoT liliwahi kuungua na kuuliza Serikali inalichukulije jambo hilo "ili Watanzania wasijeingia katika matatizo.”

Kwa pande wake, Mbunge wa Tabora Mjini (CCM), Almasi Maige alibainisha utaalamu wa BoT ni utunzaji wa fedha na si dhahabu, hivyo kuitaka Serikali ijiridhishe katika jukumu hilo jipya kwa Benki Kuu.

Kadhalika, Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Musukuma aliishauri Serikali kabla ya kuanza kutumika kwa sheria hiyo ni vyema ikaiongezea ulinzi BOT.

Mbunge wa Moshi Vijijini (Chadema), Anthony Komu alitaka kujua kama serikali imeangalia uzoefu kutoka nchi nyingine kabla ya kuandika muswada huo.

Akijibu hoja za wabunge, Prof. Kabudi aliwataka wabunge kutokuwa na hofu kuhusu usalama wa BoT kwa sababu wakati jengo linaungua lilikuwa na mbao nyingi.

Alisema teknolojia imekuwa kwa kuwekwa vifaa vya utambuzi wa moto.

Kuhusu uzoefu, Waziri Kabudi alisema wameangalia uzoefu katika nchi mbalimbali ikiwa ni pamoja na Botswana, Sierra Leone, Indonesina, Saud Arabia na Ghana.

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO KUMI YA KUFANYA KABLA YA MIAKA 25

1. Jifunze kuweka akiba ya fedha na iache bila kuigusagusa.   2. Tafuta mpenzi sahihi na tulia naye, panga maisha. 3. Ishi mahali pa peke yako, acha kuishi kwa wazazi au kupanga na nyumba na washkaji. 4. Lipa madeni yako ya zamani. Yote! 5. Tengeneza mwili ambao unataka halafu jitahidi kuu-maintain! Anza kuzingatia kuishi kwa kujali afya yako sana. 6. Jitahidi uwe na marafiki ambao wana changamoto za kimaendeleo zitakazokusaidia. 7. Anza kujinunulia assets kama ardhi na nyinginezo. 8. Jifunze kuvaa vizuri na kwa heshima, si tu ilimradi umependeza. 9. Kubali sasa kwamba umekua na acha tabia na mambo ya kitoto. 10. Yaache ya zamani yapite na anza mapya. Mwajuma huna mpango naye, achana naye. Acha kurudi rudi nyuma!

NAJIVUNIA TANZANIA

ZIJUE HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA NA WAKATI MZURI WA KUTEMBELEA   BAADHI YA HIFADHI ZA TAIFA KATIKA PICHA JINSI ZINAVYOONEKANA Na, Gordon Kalulunga WATANZANIA wengi kutokana na mazoea kuwa wanaotakiwa kutembelea hifadhi za Taifa ni watalii wa nje ya nchi, wameshindwa kujitokeza kwa wingi kutembelea hifadhi hizo kutokana na sababu mbalimbali. Moja ya sababu ya kutoweza kutembelea hifadhi hizo ni pamoja na hofu ya viingilio wakifika katika hifadhi hizo jambo ambalo naamini kuwa baada ya kusoma makala hii wengi wetu tutabadili fikra zetu na kujitokeza katika kutembelea vivutia vya utalii vilivyopo kila pembe ya nchi yetu. Baadhi ya vivutio ambavyo vinasimamiwa kikamilifu na Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) ni pamoja na hifadhi ya Taifa ya Arusha, Gombe, Katavi, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Manyara, Ruaha, Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa, Kitulo, Mkomazi na Saanane. Katika Hifadhi hizo za taifa unapotembelea kuna tozo zak...

JIFUNZE KALENDA YA UZAZI

Hii ni njia ambayo mwanamke anaweza kutumia kupanga uzazi bila kutumia dawa au kitu cha aina yoyote.  Njia hii inategemea kuchagua kwa makini siku za kufanya mapenzi kutegemeana na ufahamu wa kipindi chote cha hedhi cha mwanamke. Njia hii ina faida yake, lakini yeyote anayeitumia lazima awe makini sana, kwa sababu lazima ajue lini anategemea kupata damu ya hedhi tena.  Ni rahisi sana kufanya makosa kwa kutumia njia hii, kwa hiyo pamoja na kutoa maelezo ya jinsi ya kutumia, sisi hatumshauri mtu kutumia njia hiyo.  Nani anaweza kutumia njia ya kalenda Moja,  Wanawake walioko tayari kuchukua miezi 3 hadi 6 kupima vipindi vyao vya hedhi kabla ya kutumia njia hiyo. Pili,  Wanawake walio na mzunguko wa hedhi ambayo urefu wake haubadiliki. Tatu, Wanawake wanaojua hisabati vizuri sana.  Kwa hiyo, kabla ya kutumia njia hiyo, ni vyema kwa mwanamke kuandaa kalenda inayoonesha siku yake ya kwanza kutoa damu ya hedhi kila mwezi kwa kipindi cha miezi 3 ha...