Skip to main content

JPM ASEMA HAYA!!!!!!!!!!!

JPM Aagiza kukamatwa wanaongea ongea ovyo kuhusu Kibiti


Rais Magufuli amewaonya baadhi ya wanasiasa na kuwataka kufunga midomo yao wakati serikali inafanya kazi yake, Rais Magufuli amesema hayo leo wakati anazindua upanuzi wa bandari ya Dar es Salaam.


Rais Magufuli amewataka wanasiasa kuzungumza mambo wanayoyajua lakini si kuongea ongea tu vitu ambavyo hawavifahamu na kusisitiza kuwa baadhi ya watu ambao serikali inawashikilia katika vyombo vya usalama wanahusika na mauaji ambayo yanatokea mkoani Pwani.


"Lakini niwaombe pia na wanasiasa ambao wameshindwa ku 'contol' midomo yao na muda mwingine wanazungumza hata vitu wasivyovijua, unakuta mwanasiasa anasema watu wamekaa sana rumande anashindwa kuelewa Marekani wale watu wabaya walikaa Guantanamo miaka na miaka, lakini kwetu wanaposhikwa watu ambao wanahusika na mambo ya ajabu katika nchi kuna watu wanaongea ongea. Pwani kuna watu wamekufa kule zaidi ya 35 askari zaidi ya 15 na wanaohusika na vifo hivyo ni pamoja na hao waliopo rumande lakini mtu anatoka anasema watu wamekaa mno, unaweza kuona huyo mtu naye anahusika kwa namna moja au nyingine, wasitufanye tukafika hapo sababu wataumia, wajifunze kufunga midomo yao wakati serikali inafanya kazi yake" alisisitiza Rais Magufuli. 


Rais Magufuli anasema kumekuwa na mzaha kwa baadhi ya watu kutokana na kuhongwa pesa ndiyo maana wao kazi yao ni kupinga kila kitu. 


"Mimi nimetuma ujumbe huu ili uwafikie Watanzania na waelewe, tuna mambo makubwa tunashughulikia katika nchi hii, lakini kumekuwa na mzaha mzaha tu, unakuta muda mwingine mnashughulikia rasilimali za watanzania zinavyoibiwa , lakini unakuta mtu mwingine anapinga hadharani kwa sababu amepewa vijisenti, ninawaomba watanzania wote bila kujali itikadi za vyama vyao tutangulize masilahi ya nchi mbele, hujasimama hata siku moja kulaani mauaji yanayotokea huko halafu unaibuka unataka sifa za kisiasa eti hawa watu waachiwe, na bahati mbaya watu wanaokufa ni wa chama kimoja tu, nataka polisi mfanye kazi yenu."alisema Rais Magufuli 


Mbali na hilo Rais Magufuli amewataka polisi kuwakamata watu wote ambao wanaongea ongea juu ya mambo hayo ili walisaidie jeshi la polisi katika upelelezi, bila kuwaogopa kwa sura, wala mwendo wao.

Comments

Popular posts from this blog

NAJIVUNIA TANZANIA

ZIJUE HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA NA WAKATI MZURI WA KUTEMBELEA   BAADHI YA HIFADHI ZA TAIFA KATIKA PICHA JINSI ZINAVYOONEKANA Na, Gordon Kalulunga WATANZANIA wengi kutokana na mazoea kuwa wanaotakiwa kutembelea hifadhi za Taifa ni watalii wa nje ya nchi, wameshindwa kujitokeza kwa wingi kutembelea hifadhi hizo kutokana na sababu mbalimbali. Moja ya sababu ya kutoweza kutembelea hifadhi hizo ni pamoja na hofu ya viingilio wakifika katika hifadhi hizo jambo ambalo naamini kuwa baada ya kusoma makala hii wengi wetu tutabadili fikra zetu na kujitokeza katika kutembelea vivutia vya utalii vilivyopo kila pembe ya nchi yetu. Baadhi ya vivutio ambavyo vinasimamiwa kikamilifu na Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) ni pamoja na hifadhi ya Taifa ya Arusha, Gombe, Katavi, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Manyara, Ruaha, Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa, Kitulo, Mkomazi na Saanane. Katika Hifadhi hizo za taifa unapotembelea kuna tozo zak...

MAMBO KUMI YA KUFANYA KABLA YA MIAKA 25

1. Jifunze kuweka akiba ya fedha na iache bila kuigusagusa.   2. Tafuta mpenzi sahihi na tulia naye, panga maisha. 3. Ishi mahali pa peke yako, acha kuishi kwa wazazi au kupanga na nyumba na washkaji. 4. Lipa madeni yako ya zamani. Yote! 5. Tengeneza mwili ambao unataka halafu jitahidi kuu-maintain! Anza kuzingatia kuishi kwa kujali afya yako sana. 6. Jitahidi uwe na marafiki ambao wana changamoto za kimaendeleo zitakazokusaidia. 7. Anza kujinunulia assets kama ardhi na nyinginezo. 8. Jifunze kuvaa vizuri na kwa heshima, si tu ilimradi umependeza. 9. Kubali sasa kwamba umekua na acha tabia na mambo ya kitoto. 10. Yaache ya zamani yapite na anza mapya. Mwajuma huna mpango naye, achana naye. Acha kurudi rudi nyuma!

How to write a CV: Tips for 2018 (with examples)

When it comes to job hunting, your CV is paramount. Get it right, and you’ll have an interview in no time, but get it wrong, and you may face rejection after rejection. Every CV is different as you want to show why your set of skills makes you suitable for the position you’re applying for at that moment, but all follow a similar structure. This guide will show you how to write a great CV that’s ready for 2018 and beyond. What is a CV? Your CV, short for curriculum vitae ,  is a personal marketing document used to sell yourself to prospective employers. It should tell them about you, your professional history and your skills, abilities and achievements. Ultimately, it should highlight why you’re the best person for the job. A CV is required when applying for a job. In addition to your CV, employers may also require a cover letter and a completed application form( Browse CV templates ) What to include in your CV in 2018 While the structure of a CV is flexible, bending t...