Skip to main content

CHUKUA TAHADHARII!!!!!!!!!!!

Chukua Tahadhari Kama Unatumia Hizi Bulb

Tunapenda kupunguza matumizi ya nishati, hizi bulb ambazo ni rafiki wa mazingira na zinazookoa nishati(energy serving bulb) zimekuwa zikitumika zaidi kwa sasa.

Ila ni vyema ujue kwamba hizi bulb za kisasa ni kweli zina sumu. Shirika la kulinda Mazingira limetoa maelekezo ya dharura unayohitaji kuyafuata endapo bulb yako itavunjika.

Hii ni kutokana na gesi yenye sumu inayotoka endapo bulb itavunjika.

Taasisi ya Fraunhofer Wilhelm Klauditz ya Ujerumani inadai kuwa kama taa hii itavunjika ndani ya nyumba itatoa mara 20 zaidi ya Mercury katika hewa

Bulb hizi za kupunguza matumizi ya Nishati zinaweza kukuletea matatizo haya;

  • Kizunguzungu
  • Kifafa
  • Maumivu ya kichwa
  • Uchovu
  • Kutostahimili
  • Wasiwasi


1.Bulbu hizi zinazookoa nishati zina wingi wa zebaki(mercury)

Mercury ni hatari hasa kwa 

  • watoto na 
  • wanawake wajawazito. 
  • Uharibu mfumo wa neva, 
  • ubongo, 
  • figo na 
  • ini.
  • Pia uharibu uzazi, 
  • kinga ya mwili, 
  • mfumo wa mishipa ya moyo,
  • pia inaweza kukusababishia mitikisiko,
  • kukosa usingizi, kuumwa kichwa, 
  • wasiwasi na 
  • kupoteza kumbukumbu 


2.Bulb hizi zinaweza kukusababishia Kansa
  • Utafiti uliofanywa Maabara uligundua kwamba hizi balbu pia zina sumu zinazoweza kukusababishia kansa
  • Phenol, tindikali hii yenye chembechembe nyeupe zenye sumu inapatikana katika makaa ya mawe na inatumika kwa matumizi ya viwanda
  • Taa hizi zina wingi wa mionzi ya UV
  • Mionzi hii ya UV si mizuri kwa afya ya ngozi na inaweza kukusababishia kansa ya ngozi.


Baada ya kusoma haya maelezo unaweza kuchagua kuendelea kutumia balbu hizi kwa maana gharama zake ni nafuu, kama utafanya hivyo basi yakupasa kusoma maelekezo na kujua jinsi ya kukabiliana na mercury(zebaki) na kemikali zinazoweza kukusababishia kansa.

Fanya hivi kabla ya kutoa bulb iliyopasuka;


  • Watu na wanyama waondoke katika chumba
  • Fungua madirisha na milango kwa mda wa dakika 5-10

Comments

Popular posts from this blog

Aina bora za ng’ombe wa maziwa, banda na namna ya kuanza ufugaji

Uzalishaji wa maziwa ni biashara nzuri sana na ya kuvutia ambayo huwa na faida nyingi na humfanya mfugaji kuridhika hasa kwa yule anayependa kazi hii. Hata hivyo, ni lazima kuanza kwa kuweka msingi imara hata kabla ya kufikiria ni aina gani ya mbegu utaichukua kwa ajili ya kufuga. Ni vizuri kufahamu kuwa, usimamizi ni moja ya jambo muhimu sana ambalo likifanyiwa uzembe linaweza hata kumbadilisha ng’ombe wa maziwa kuwa na uzalishaji duni kama ngo’mbe wa kienyeji. Aina mbalimbali za ng’ombe wa maziwa huwa na mahitaji tofauti, hivyo kiwango cha maandalizi yako ni muhimu sana. Unahitajika kufahamu kuwa, unalazimika kufikia mahitaji yako kwa ajili ya lishe, si kwenye mahitaji ya awali tu bali pamoja na mahitaji ya baadaye ya ngo’mbe wako. Suala hili limefanya wafugaji wengi kushindwa kuendelea kutokana na kuwa hujiingiza katika shughuli hii bila kuangalia mambo ya msingi yanayotakiwa pamoja na kuweka mipango thabiti. Pamoja na kuwa mahitaji yote kwa ajili ya lishe na mambo me...

NAJIVUNIA TANZANIA

ZIJUE HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA NA WAKATI MZURI WA KUTEMBELEA   BAADHI YA HIFADHI ZA TAIFA KATIKA PICHA JINSI ZINAVYOONEKANA Na, Gordon Kalulunga WATANZANIA wengi kutokana na mazoea kuwa wanaotakiwa kutembelea hifadhi za Taifa ni watalii wa nje ya nchi, wameshindwa kujitokeza kwa wingi kutembelea hifadhi hizo kutokana na sababu mbalimbali. Moja ya sababu ya kutoweza kutembelea hifadhi hizo ni pamoja na hofu ya viingilio wakifika katika hifadhi hizo jambo ambalo naamini kuwa baada ya kusoma makala hii wengi wetu tutabadili fikra zetu na kujitokeza katika kutembelea vivutia vya utalii vilivyopo kila pembe ya nchi yetu. Baadhi ya vivutio ambavyo vinasimamiwa kikamilifu na Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) ni pamoja na hifadhi ya Taifa ya Arusha, Gombe, Katavi, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Manyara, Ruaha, Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa, Kitulo, Mkomazi na Saanane. Katika Hifadhi hizo za taifa unapotembelea kuna tozo zak...

Mawazo Yakinifu Ya Mafanikio Endelevu Kwako

Mafanikio yoyote yanaanza na mawazo. Hakuna mafanikio yanazaliwa nje ya mawazo. Kwa jinsi unavyokuwa na mawazo bora ndivyo unavyozidi kuwa na mafanikio bora kwako. Mawazo bora unayapata vipi, unayapata kwa kujifunza. Kupitia makala haya, nakukaribisha tujifunze pamoja mawazo yakinifu ya mafanikio yako endelevu. Naamini kupitia mawazo haya, utajifunza kitu ambacho kitakutoa hatua moja na kwenda hatua nyingine, karibu tujifunze. 1.Unaweza ukaendelea kuteseka kila siku na maisha na kuteseka kila na kila aina ya ugonjwa, lakini hiyo yote inaweza ikasababishwa na ujinga ambao  umeushikilia. Ujinga ni adui mkubwa sana wa mafanikio yako. Fanya ufanyalo, futilia mbali ujinga wote ambao upo kwako. Ukifuta ujinga utakuweka huru na utaishi maisha ya mafanikio. Wajinga ndio waliwao na ujinga haumfanikishi mtu, tadhari usiwe kichaka cha ujinga, UTAKWAMA. 2. Kwa mawazo uliyonayo ujue kabisa yanatengeza dunia yako, yanatengeneza maisha yako au yanaumba maisha yako. Swala la kuwa makini sana kw...